Katika kusaidia kufanikiwa kwa agenda ya serikali ya kupunguza matumizi ya mkaa unaotokana kwa kukatwa kwa miti jumla ya wakina mama lishe 100 wamefanikiwa kupata elimu ya kutumia nishati ya mkaa ujulikanao kwa jina la Brikwiti utokanao na mabaki ya taka ikiwemo yatokanayo na mimea.
Teknolojia hiyo ya utengenezaji wa nishati mbadala imetambulishwa hapa nchini na taasisi kutoka Norway ya Norges Vel ambayo ilishirikiana na IMED Foundation ambao ndio wamesambaza elimu kwa akina mama hao lengo ikiwa ni kukabiliana na uharibu wa mazingira ambao umekuwa ukijitokeza kutokana na kasi ya ukataji miti ovyo kwa ajili ya kutengeneza mkaa na kuni huku kundi la mama lishe likitajwa kuongoza matumizi ya nishati hiyo.
Mkurugenzi wa IMED Foundation - DK. Donath Olomi
Msimamizi wa mradi wa Norges Vel - Neatness Bwege
Wakizungumzia teknolojia hiyo Msimamizi wa mradi huo Neatness Bwege na Mkurugenzi wa IMED Foundation DK. Donath Olomi wamesema licha ya nishati hiyo kupunguza uharibifu wa mazingira pia inapunguza gharama za matumizi wa mkaa wa utokanao na miti.
Mkaa awa Brikwiti hutengenezwa na mabaki ya mimea mikavu mfano, pumba za mpunga, malanda, maganda ya karanga, miwa ambayo husindikwa kwa kutumia mashine maalumu.
Mwenyekiti wa mama lishe mkoa wa Dar es Salaam Bi. Mwanahamisi Mwendero
Pia Mwenyekiti wa mama lishe mkoa wa Dar es Salaam Bi. Mwanahamisi Mwendero amesema matumizi ya mkaa huo wa Brikwiti ni mazuri na unaweza kukaa na moto mpaka masaa 6 bila kuzima na pia ni mzuri kwa afya maana hauna moshi.
Teknolojia hiyo ya utengenezaji wa nishati mbadala imetambulishwa hapa nchini na taasisi kutoka Norway ya Norges Vel ambayo ilishirikiana na IMED Foundation ambao ndio wamesambaza elimu kwa akina mama hao lengo ikiwa ni kukabiliana na uharibu wa mazingira ambao umekuwa ukijitokeza kutokana na kasi ya ukataji miti ovyo kwa ajili ya kutengeneza mkaa na kuni huku kundi la mama lishe likitajwa kuongoza matumizi ya nishati hiyo.
Wakizungumzia teknolojia hiyo Msimamizi wa mradi huo Neatness Bwege na Mkurugenzi wa IMED Foundation DK. Donath Olomi wamesema licha ya nishati hiyo kupunguza uharibifu wa mazingira pia inapunguza gharama za matumizi wa mkaa wa utokanao na miti.
Mkaa awa Brikwiti hutengenezwa na mabaki ya mimea mikavu mfano, pumba za mpunga, malanda, maganda ya karanga, miwa ambayo husindikwa kwa kutumia mashine maalumu.
Mwenyekiti wa mama lishe mkoa wa Dar es Salaam Bi. Mwanahamisi Mwendero
Pia Mwenyekiti wa mama lishe mkoa wa Dar es Salaam Bi. Mwanahamisi Mwendero amesema matumizi ya mkaa huo wa Brikwiti ni mazuri na unaweza kukaa na moto mpaka masaa 6 bila kuzima na pia ni mzuri kwa afya maana hauna moshi.
Utambulishaji wa Mkaa wa Brikwiti nchini Tanzania
Reviewed by Unknown
on
September 18, 2017
Rating:

No comments: