Kampuni ya Sokabet imezinduliwa rasmi jana ambapo itakuwa inajihusisha na michezo ya kubashiri matokeo (kubet) ambayo nia yake kubwa ni kuwawezesha Watanzania kupata fedha, kukuza michezo na kuchangia maendeleo mbalimbali ya kijamii.
Kampuni hiyo ya Kitanzania yenye
maskani yake jijini Dar es Salaam itawawezesha washiriki kubashiri matokeo
kupitia tovuti yake ya www.sokabet.co.tz ambapo washiriki wanaweza kuvuna fedha
nyingi hadi shilingi milioni 100 kwa kubet kwa shilingi 1,000 tu.
Licha ya Sokabet kuwawezesha washiriki
wenye umri wa kuanzia miaka 18 kubet pia inayo nafasi ya kukuza michezo kwa
kuwekeza katika taasisi mbalimbali mfano kwa kuanzia imeanza na Klabu ya
Majimaji ya Ruvuma.
Sokabet inakuwa mmoja wa wadhamini wa
Majimaji, klabu inayoshiriki katika Ligi Kuu Tanzania Bara ambapo itatoa
mamilioni ya shilingi katika ufadhili huo ikiwa ni sehemu ya kurejesha kile
inachokipata kwenye jamii.
Mshambuliji wa Kimataifa aliyewahi
kutamba pia na timu ya Taifa ya Tanzania ambaye kwa sasa anaitumikia
timu ya MajiMaji ya Songea Danny Mrwanda, ametamba kwamba baada ya klabu
yao kupata udhamini mnono wa milioni 150, kutoka Soka Bet sasa wao ni
kucheza Kandanda ili kupata matokeo.
Kauli hiyo ameitoa wakati viongozi wa klabu yake walivyokuwa wakisainiana mkataba wa kudhamini klabu yao kwa mwaka mmoja ,ambapo mekiri sasa ,kazi iliyobaki ni kusakata kandanda pekee Uwanjani.
Nyota huyo aliyewahi kung'ara zaidi kimataifa ,amesema kikosi cha Maji Maji msimu huu kimeandaliwa vyema na wapo katika kuhakikisha wanapambana katika,Ligi Kuu ya Tanzania Bara hadi kieleweke.
Kauli hiyo ameitoa wakati viongozi wa klabu yake walivyokuwa wakisainiana mkataba wa kudhamini klabu yao kwa mwaka mmoja ,ambapo mekiri sasa ,kazi iliyobaki ni kusakata kandanda pekee Uwanjani.
Nyota huyo aliyewahi kung'ara zaidi kimataifa ,amesema kikosi cha Maji Maji msimu huu kimeandaliwa vyema na wapo katika kuhakikisha wanapambana katika,Ligi Kuu ya Tanzania Bara hadi kieleweke.
Kampuni ya Sokabet Imezinduliwa Rasmi Jana
Reviewed by Unknown
on
September 04, 2017
Rating:

No comments: