Michezo ni Ajira ya Kudumu-Waziri Mwakyembe

Waziri wa Habari Utamaduni,Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe amesema Serikali iko teyari kuunga mkono na kusaidia wanamichezo pia na kuboresha michezo mashuleni na kuwasii kuongeza juhudi na kuzidi kupambana kwani michezi ni ajira ya kudumu.

Waziri wa Habari Utamaduni,Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe akizungumza wa waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam.

Akiongea na waandishi wa habari wakati akiwapongeza baadhi ya wanamichezo walioshiriki mashindano ya shule za sekondari Afrika Mashariki yaliyofanyika nchini Uganda wakati wachezaji hao wamerejea nchini na Medali 10 huku mshiriki mwenye umri wa miaka 16 Winfrida Makenji akitwaa medali nne katika michezo tofauti tofauti ya riadha.

Katika hatua nyingine Waziri huyo amesisitiza kuwaunga mkono walimu mashuleni kwa kuwalea vizuri wanafuzi hao wenye vipaji mashuleni kwani vipaji hivyo wamevilea na sasa matunda yake yanaonekana kuwa makubwa, na ameongeza kwa kusema Serikali itafanya mpango mzuri wa kuhakikisha mwakani wanapeleka washiriki wengi katika mashindano hayo ambayo yanatarahjiwa kufanyika Rwanda.

Mashindano hayo yanaheshima kubwa katika Afrika mashriki na vijana hao wamefanya kazi kubwa ambayo imeonekana kuleta matunda mazuri.
Michezo ni Ajira ya Kudumu-Waziri Mwakyembe Michezo ni Ajira ya Kudumu-Waziri Mwakyembe Reviewed by Unknown on August 30, 2017 Rating: 5

2 comments:

  1. Hi this is impressive. I am confident this blog will grow in both popularity and fame

    ReplyDelete
  2. God speed my brother, i see the future in you.

    ReplyDelete

Chips Mayai Ni Hatari Kwa Afya Yako

Ulaji wa chips umetajwa kuwa hatari kwa afya ya Binadamu, kwani husababisha maradhi mengi yasiyo ya kuambukiza hasa figo, moyo, shinikizo...

Powered by Blogger.